News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Tuesday, 3 October 2017

JULIO SI MZEE WA MANENO YA KUUMA?? MASHABIKI MWANZA WAMPA MINENO YA KUUDHI MPAKA KALALAMIKA!!

     
Mwanza. Mashabiki wa timu ya Alliance SC waliwacheka wachezaji wa Dodoma FC  kwa kuwaita madingi jambo ambalo lilimkera Kocha Jamhuri Kihwelu “Julio”na kutamka neno nzito.
Alliance ilikuwa mwenyeji wa Dodoma FC katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza uliopigwa Uwanja wa Nyamagana juzi na ambapo Alliance ilishinda bao 1-0.
Julio alisema licha ya wachezaji hao kucheza muda mrefu, lakini wana uwezo mkubwa uwanjani ambapo kama wangekuwa wazee basi wangekuwa kila mechi wanafunga mabao saba.
“Hakuna wazee kwenye timu yangu hawa ni wachezaji ambao wamecheza soka siku nyingi lakini wana uwezo mkubwa wa kucheza mpira kama wangekuwa madingi si tungepigwa saba na Alliance”alisema Julio.
Julio alisema hawa hawa wachezaji  wazee wanaowasema ndio watakaipandisha  Dodoma FC Ligi Kuu msimu ujao.
USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment