Bondia Conor McGregor ameahidi kumshinda Mpinzani wake Floyd Mayweather ndani ya Raundi nne katika Pambano lao litakalofanyika Agosti 26 Mwaka huu Mjini Los Angels nchini Marekani.
Mayweather,4o pamoja na McGregor wamekutana kwa mara ya Kwanza Mjini Los Angels katika Mkutano mbele ya Waandishi wa Habari na mamia ya watu huku wakijinadi na kutambia kabla ya Pambano lao la kihistoria la uzito wa Kati.
“Miguu yake midogo, akili yake ndogo na Kichwa chake kidogo. Ntampiga ndani ya Raundi ya nne, atapoteza fahamu mapema tu, Mwendo wake na anavyoonekana hataniweza kabisa”. Alisema Bondia McGregor mbele ya Mamia ya watu na waandishi wa Habari.
Kwa upande wake Bondia Floyd Mayweather ambaye ni Mshindi mara tano wa Ubingwa wa Dunia kwa Uzito wa Kati amesema Licha ya umri wake na kuonekana amechoka ameahidi kumshinda McGregor ambaye hajawai pigana Pambano la Kimataifa.
Floyd Mayweather na Conor McGregor wanakutana kwa mara ya kwanza Ulingoni katika Pambano lao litakalopigwa Agosti 26 mwaka huu 2017 Mjini Los Angels nchini Marekani. Mayweather atashuka kwenye Pambano hilo akiwa na Historia ya kutopoteza Mchezo wowote huku Conor McGregor akiwa amepoteza Michezo mitatu katika Michezo 26 aliyocheza.
0 comments :
Post a Comment