Katika hali ambayo inaonyesha kua kuna mfukuto wa chini kwa chini kwenye Klabu Ya simba hali iliyopelekea kuzuka makundi mawili ya wanachama kundi moja likiitwa SIMBA ASILI na SIMBA MHINDI. Mwanachama maarufu wa Simba anaefahamika kwa jina la Bi Chuma au maarufu kwa jina la Bi Hindu amewa washia moto wa Gesi viongozi ambao wameitisha mkutano na kuwaambia wawe na utu wakati wenzao wako ndani wao kwa uroho wa madaraka na wa hela kutoka kwa aliemuhita muhindi wanaitisha mkutano ili wafanye mabadiliko wanayoyataka huku viongozi waliowaweka hapo walipo wako ndani akaendelea kuhoji wao waliokua nje roho zinawauma iweje wanaoshinda nao oficn wawe hawana hata roho ya huruma Bi hindu alizidi kuuwasha moto ambao ambao inaonekana ni Dongo kwa Msemaji wa Simba kua Tabia ya yeye akiongelea maswala ya Simba wanaanza kumwambia ooooh! Bi Hindu umezidi ngenga uolewe kama ndoa ni mali akamlete baba yake amuoe☺☺!! baada ya mazungumzo hayo Radio hii ikampigia simu Haji Manara kuhusu Maongezi na malalamiko ya Bi hindu msemaji wa Simba hakua kama yule tunaemjua ambae halalagi na Deni alipoulizwa alisema tu kwa kifupi itakapohitajika kulitolea ufafanuzi tutalitolea tu mwandishi wa 24RADIO akazidi kumuuliza je mkutano uko pale pale? aaaah nimekwambia hiviiiiii ...tiiii.. tiiii ..tiii.. tiiii...Manara Haji akawa amekata simu leo hakua na Maneno ya majigambo kama kawaida yake hii ikiwa na Maana kua Bi hindu amemkata umeme
0 comments :
Post a Comment