
Klabu ya Yanga imetoa tamko kuhusu taarifa za kutaka kuondoka kwa beki wao wa pembeni Haji Mwinyi ambaye anahusishwa kuondoka klabuni hapo hasa baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika michuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika nchini Kenya mapema mwezi huu.
Mwinyi amekuwa hana uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza cha Yanga, hali ambayo inadaiwa imechangia kwa mchezaji huyo mwenyeji wa Zanzibar kuwa na nia ya kuondoka. Yanga wamekiri kupokea barua ya Haji Mwinyi akiomba kuondoka pia Baba yake mzazi alikwenda klabuni hapo kwa ajili ya kulitilia mkazo swala hilo Yanga wamesema wamemjibu kua suala la kuondoka Yanga n suala la kuvunja mkataba kwa hio taratibu za kuvunja mkataba zipo ila wamemshauri ingekua busara angetulia kwa kua bado anahitajika kwenye kikosi pia kocha ameona kiwango chake kwenye mashindano kule kenya na azidishe mazoezi kocha lazima atampanga tu kuliko suala la kufkiria kuvunja mkataba
USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA



0 comments :
Post a Comment