News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Thursday, 30 November 2017

PIGO ARSENAL: LACAZETTE KUIKOSA MAN UNITED JUMAMOSI

Tokeo la picha la lacazette
Mshambuliaji raia wa Ufaransa Lacazette anaekipiga na Arsenal ataikosa mechi muhimu dhidi ya Manchester United baada ya kuumia nyonga katika mchezo wa jana jumatano dhidi ya Huddersfield.
Arsenal katika mchezo huo wakicheza soka safi waliweza kuibuka na ushidi wa goli 5-0 ikiwa ni onyo kwa mashetani hao wa Old Traford watakaokutana nao jumamosi hii. Alexndre Lacazette dakika tu ya tatu ya mchezo akipokea pasi nzuri ya Ramsey aliweza kufunga goli zuri na kuwatanguliza mbele Arsenal likiwa goli lake la saba katika ligi .
Lacazette alitolewa kipindi cha mapumziko baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Olvier Giroud aliyeweza kuwapa Arsenal magoli mawili akiwa katika kiwango bora zaidi.
Magoli mengine ya Arsenal yalifungwa na Mesut Ozil na Alex Sanchez

USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment