News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Thursday, 10 August 2017

SIRI YAVUJA: YANGA WAMTUMIA IBRAHIM AJIB KUWASOMA SIMBA ILI ........

Wakati wapenzi wa SIMBA wakiwa na furaha kuhusiana na Tamasha la Simba Day lilivyokwenda na matokeo yake ikiwa pamoja na kuwaona wachezaji wao wapya waliosajiliwa na ikiwemo na matokeo ya mtanange uliopigwa siku ya simba Day lakini kuna kitu kimoja kilichotokea ambacho kiliwaacha hoi wapenzi wa soka  Tanzania ikiwa ni kinyume kabisa za utaratibu wa vilabu hivi viwili ambapo mchezaji ambae aliondoka Simba msimu huu huu akaenda kwa mahasimu wao YANGA  Ibrahim Ajib kwenda kwenye SIMBA DAY huku sakata lake likiwa hata halijaisha vizuri tumeshuhudia vijembe ambavyo Ajib anavitoa Twitter pia tumekua tukishuhudia pia Msemaji wa Simba Haji Manara vijembe alivyokua akivitoa kwake acha matusi na kashfa ambazo Ajib anavipata kila siku kwenye mitandao ya kijamii hasa Facebook kwenye Group za mashabiki wa simba lakini Ajibu akaenda, je ni kipi ambacho kilimsukuma Ibrahim Ajibu  aende bila kuogopa ajira yake mpya ambayo hata hajaanza kuitumikia kwenye mechi za ligi? katika kuchimbua swala hili MWANASPORTS LEO
lilipata jibu kwa mtu ambae hakutaka kutajwa jina lake kua ule ulikua mpango wa kikosi cha Yanga
kuwasoma wapinzani wao na mtu anaekifahamu vizuri kikosi hicho ni Ibrahim Ajibu kwa hio lile lilikua jicho la YANGA kuwasoma SIMBA na kufahamu udhaifu na uimara wao  na YANGA wamefanikiwa kwa hilo wakati mashabiki wa SIMBA wakichekelea ooooh! Ajibu ameanza kuimiss SIMBA  kumbe Ajib amefika na yake na amepata alichokitaka na kukipeleka kwa kocha wake Lwandamina  hivi mpenzi msomaji wa blog hii ya Mwanasports leo  nadhani unazijua timu hizi mbili zilivyo tena wakiwa wanakaribia mechi baina yao ingekua Ajib ameenda tu mwenyewe  angekua na kibarua leo hii YANGA?  au viongozi wa timu ya YANGA wangekaa tu kimya kama hivi Haji Manara anapiga madongo wao wamekaa kimya  bila kuongea chochote huku kukiwa na ushahidi wa picha kila sehemu? mpira ni mipngo na kwenye hili YANGA wamewini sasa tuone je ujanja waoutawasaidia  tarehe 23 watakapokutana?
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment