Simba iliachana na Manyika na kipa wake mwingine mdogo, Dennis Richard iliyempandisha kutoka timu B, baada ya kuwasajili kwa mpigo makipa namba moja na namba mbili wa timu ya taifa, Taifa Stars, Aishi Manula kutoka Azam FC na Said Mohammed kutoka Simba SC.
Manyika aliyesajiliwa Simba SC Julai mwaka 2014, amedaka jumla ya mechi 51 za mashindano tofauti, nyingi za kirafiki akifanikiwa kusimama langoni mara 30 bila kuruhusu nyavu zake kuguswa huku akiwa amefungwa jumla ya mabao 34.
Singida United anakwenda kukutana na makipa wengine watatu, wakiongozwa na mkongwe Ally Mustafa ‘Barthez’ pamoja na Said Lubawa na Benedicto Tinocco, ambao wote ni mahiri pia.


0 comments :
Post a Comment