News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Monday 21 August 2017

BREAKING NEWS: PIUS BUSWITA AFUNGIWA BAADA YA KUSAINI SIMBA NA YANGA

Ikiwa Kamati ya KatibaSheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ilikuwa katika kikao cha kupitisha usajili ambacho kimefikia tamati leohabari za uhakika kutoka ndani ya TFF zinaeleza kuwa Kiungo wa YangaPius Buswita amefungiwa kuitumikia timu hiyo kutokana na Simba kumwekea pingamizi.
Simbawalimwekea pingamizi Buswita wakidai alisaini katika timu yao kabla ya kusaini Yanga akitokea Mbao FC ya Mwanza.
Ikumbukwe mwishoni mwa mwezi Juni,Simba walitangaza kumsainisha Buswita kabla ya kuibukia Yanga ambayo walimpa mkataba wa miaka miwili.
Mtoa habari huyo alidadavua kuwa kama Yanga watataka kumtumia Buswita basi wamalizane na Simba ambayo fedha walizotanguliza kutaka kumsajili hazijarudishwa.
Hivyo basiKamati hiyo kesho itaeleza suala hilo la Buswita ambaye anaweza akakosa katika mchezo wa Jumatano dhidi ya mahasimu wao,Simba.
* USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA*
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment