Soka la Tanzania limekumbwa na mtikisiko mkubwa baada ya rais na makamu wake wa shirikisho TFF, Jamal Malinzi na Celestin Mwesigwa kupandishwa kizimbani kujibu kashfa zinazowakabili.
Kadhalika rais wa Simba, Evans Aveva na msaidizi wake Nyange Kaburu walifikishwa mahakamani kutokana na tuhuma za ufisadi.
Kupitia akaunti yake ya instagram msemaji wa Simba, Haji Manara amewataka wapenzi na mashabiki wa Simba kuwa watulivu kipindi hiki kufwatia raisi na makamu wake kushikiliwa kutokana na kashfa ya ufisadi.
"Tuwe watulivu wana Simba Sc...pole sana Raisi na makamu, tunaamini mtavuka salama mtihani huu" aliandika hivyo Haji Manara.
Raisi wa Simba Evans Aveva na makamu wake Nyange Kaburu, wanakabiliwa na makosa matano ya kutakatisha dola 300,000
0 comments :
Post a Comment