News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Wednesday 19 July 2017

NEYMAR AKUBALI KUTUA PSG AKIRI HADHARANI: NA PSG WASEMA....


MSHAMBULIAJI Neymar amekubali ofa ya Paris Saint-Germain kumuhitaji kwa dau la Pauni Milioni 195, kwa mujibu wa taarifa nchini Brazil.  
Chaneli ya micheo ya Brazil, Esporte Interativo imeripoti kwamba nyota huyo wa Barcelona amekubaliana vipengele vya mkataba na PSG kuelekea uhamisho wa rekodi kubwa ya dunia, Pauni Milioni 195.
PSG imejibu taarifa hizo kwa kuliambia gazeti la L’Equipe jana kwamba ni kweli wanamtaka Neymar, lakini hawajatoa ofa iliyotajwa.
Mapema Jumatatu, gazeti la michezo Barcelona, Sport liliripoti likiwanukuu watu wa karibu wa Mbrazil huyo kwamba ‘hana furaha’ katika klabu hiyo, kwa sababu anabaki kwenye kivuli cha akina Leo Messi na na Luis Suarez.
Barcelona nayo inamtaka kiungo Mtaliano wa PSG, Marco Veratti ambaye dau lake ni Pauni Milioni 88. 

 SHARE HABARI ILI WATU WENGI WAIONE BONYEZA SHARE KWA FACEBOOK HAPO CHINI
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment