News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Monday 17 July 2017

MSAMAHA WANUKIA VIFUNGO VYA DK NDUMBARO, HAJI MANARA


Kamati ya nidhamu ya TFF ambayo imeundwa hivi karibuni, huenda ikatoa msamaha kwa wale waliokuwa wamefungiwa.

Taarifa za ndani zinaeleza, Haji Manara na Dk Damas Ndumbaro ambao walifungiwa kwa figisu wanaweza kusamehewa.

“Kumekuwa na vikao kuangalia mambo yalivyokwenda na ilionekana kuwa Ndumbaro, Manara na hata Jerry Muro ambaye anamalizia adhabu yake walifungiwa kimakosa.

“Huenda wakaunguliwa, lakini ni suala la kusubiri tu,” kilieleza chanzo kutoka TFF.

Wote walifungiwa na utawala wa Malinzi ingawa walilalamika kwamba kufungiwa kwao ilikuwa ni suala la uonevu wa wazi.
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment