News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Saturday, 16 December 2017

SIMBA YACHEMKA KWA ASANTE KWASI:MKATABA NA LIPULI WAHARIBU TUKIO

Image may contain: one or more people and people sitting
Simba inaonekana kama imekwama kumsajili beki Asante Kwasi.

Taarifa zinasema, Simba imegundua Kwasi ana mkataba wa miezi saba na Lipuli ya Iringa, jambo ambalo limewakatisha tamaa.

Simba ilikuwa imemficha Kwasi jijini Dar es Salaam kusubiri kumalizana naye baada ya wakala wake kusema hakuwa na mkataba na Lipuli.

Lakini baada ya kufanya uchunguzi wa kina kupitia kamati yake ya usajili, iliamua kufunga breki ili kutafakari kwanza kuangalia kama inawezekana kujadiliana na Lipuli au kuachana naye.

Dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufungwa saa sita na dakika moja, na inaonekana umebaki muda mchache Simba kumaliza na Lipuli ingawa ilielezwa kuna juhudi zilikuwa zinafanywa.
USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment