Sakata la mwanasheria Tundu Lisu kushambuliwa kwa risasi bado ni gumzo nchini Tanzania.
Mwanasheria huyo ambaye pia ni mbunge alikutwa na tukio hilo juzi Alhamisi alipokuwa akielekea nyumbani kwake Area D mkoani Dodoma akitokea bungeni.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara naye alitoa maoni yake juu ya hicho kilichotokea.
Manara kaandika haya: “Mimi ni Mwanaccm kindakindaki na sina haya kwenye hili, ila mimi ni Mtanzania zaidi kuliko itikadi yangu, naomba uzima wa afya ya mh Tundu Lisu @tundulissutz, upone haraka bro, muhimu tuache vyombo vije kutupa uchunguzi wao.”

* USISAHAU KULIKE PAGE YETU HAPA*
Millionaire  Ads




0 comments :
Post a Comment