Ajibu
amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili na ametambulishwa leo Jumatano
mbele ya Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa katika makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo
Jangwani jijini Dar.
Yanga
imefanikiwa kuinasa saini ya Ajibu baada ya mchezaji huyo kushindwa kuafikiana
na uongozi wa klabu yake ya zamani katika makubaliano ya mkataba mpya.
Ajibu
anakuwa mchezaji wa tatu kusajili na kutambulishwa na Yanga katika kipindi hiki
baada ya awali klabu hiyo kumsajili beki wa Taifa Jang’ombe, Abdallah Haji ‘Ninja’
na kiungo wa Mbao FC, Pius Buswita
0 comments :
Post a Comment