Mwanza. Mdogo wa winga wa Yanga, Simon Msuva mshambuliaji James Msuva amejiunga na klabu ya Mbao FC.
Mshambuliaji huyo chipukizi amefanya mazoezi na Mbao iliyojichimbia katika uwanja wake wa nyumbani uliopo Mjini Mwanza.
Katika mazoezi hayo James alikuwa na wachezaji mwingine Amos Abel, aliyewahi kuichezea timu ya vijana ya Yanga na Kipa Kabali Faraji aliyewahi kuichezea klabu ya Simba na African Sports iliyoshuka Daraja.
Wachezaji hawa wamefanikiwa kuingia moja kwahiyo moja katika mipango ya kocha Etienne Ndyaragije baada ya kipindi chote cha mchujo walichokuepo Mwanza takribani wiki sasa.
0 comments :
Post a Comment