
Alexis Sanchez akikimbia kushangilia baada ya kiungo wa PSG, Marco
Verratti kujifungia kuipatia bao la pili Arsenal dakika ya 60 lililoelekea kuwa la ushindi kabla ya PSG kusawazisha na mchezo huo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Playa kumalizika kea are ya 2-2 Uwanja wa Emirates. Bao lingine la Arsenal lilifungwa na Olivier Giroud dakika ya 45, wakati ya PSG yalifungwa na Edinson Cavani dakika ya 18 na Alex Iwobi dakika ya 77 aliyejifunga pia. Kwa matokeo hayo, Arsenal na PSG zote zimesonga mbele kutoka kundi hilo PICHA ZAIDI BONYEZA HAPA!!
MATOKEO YA MAN CITY

Kiungo wa Hispania David Silva (kulia) akiushuhudia mpira alioupiga ukielekea
nyavuni dakika ya 45 na usher kuipatia Manchester City bao la kusawazisha katika sare ya 1-1 na wenyeji, Borussia Monchengladbach Uwanja wa Borussia-Park mjini Monchengladbach katika mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bao la wenyeji lilifungwa na Raffael dakika ya 23 PICHA ZAIDI BONYEZA HAPA
MATOKEO YA ATLETICO MADRID

Antoine Griezmann akipongezwa baada ya kuifungia bao la pili Atletico Madrid katika ushindi wa 2-0 dhidi ya PSV Eindhoven kwenye mchezo wa Kundi D Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Vicente Calderon mini Madrid haiku wa jana. Bao lingine la Atletico ambayo inaungana na Bayern Munich kusonga mbele kutoka kundi hilo lilifungwa na Kevin Gameiro PICHA ZAIDI HAPA
0 comments :
Post a Comment