News
Loading...
Image Map HII NI 24 RADIO SIKILIZA NA UTUTUMIE SMS KWENDA 0684 666320 KUHUSU UNAVYOTUSIKIA

Thursday, 24 November 2016

BALE NJE WIKI KADHAA AKOSA MECHI YA EL CLASICO

WINGA Gareth Bale ataikosa mechi ya mahasimu wa Hispania, El Clasico Desemba 3 baada ya Real Madrid kuthibirisha ameumia kifundo cha mguu wa kulia. 
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 pia yuko hatarini kuukosa mchezo mwingine wa Madrid na Borussia Dortmund kuwania usukani wa kundi katika Ligi ya Mabingwa.
Na wakati wanatoa taarifa hiyo leo, dawati la tiba la klabu lilikuwa halijakamilisha vipimo ili kujua kama atahitaji upasuaji, lakini limehakikisha atacheza Klabu Bingwa ya Dunia mwezi ujao. 

Nyota wa Real Madrid, Gareth Bale atawakosa Barcelona Desemba 3 katika mechi ya El Clasico 

Real Madrid wataanzia katika Nusu Fainali ya michuano hiyo nchini Japan Desemba 15 na wangependa mchezaji wao huyo wa pili kulipwa vizuri baada ya Cristiano Ronalo awepo.
Share on Google Plus

About

0 comments :

Post a Comment